Magonjwa ya kwenye maji ni magonjwa yanayopatikana ama kusambazwa kupitia maji. Magonjwa haya ni kama vile homa ya matumbo, kipindupindu, kuhara na kuhara damu. Kama maji si safi na salama kwakuwa yamechanganyikana na maji taka basi kuna uwezekano mkubwa wa mtumiaji kupata maambukizi.
Kinga[edit | edit source]
Inashauriwa kuchemsha maji au kuyavukiza kabla ya kuyatumia ili kuhakikisha maji ni safi na salama. Pia maji huweza kufanywa safi na salama kwa kutumia dawa kama waterguard.